Kitengo cha ibada:

Jawabu: Mola wangu ni Mwenyezi Mungu aliyenilea na akalea watu wote kwa neema zake.
Na ushahidi ni kauli yake Mtukufu:
"Shukurani zote njema anastahiki Mwenyezi Mungu mola wa viumbe vyote" [Suratul Fatiha: 2]

Jawabu: Dini yangu ni uislamu: Nao Ni kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kumpwekesha, na kunyenyekea kwa kumtii, na kujiepusha na ushirikina pamoja na washirikina.
Amesema Allah Mtukufu:
"Hakika dini inayo kubaliwa kwa Mwenyezi Mungu ni Uislamu" [Surat Al Imran: 19]

Jawabu: Ni Muhammad Rehema na Amani ziwe juu yake.
Amesema Allah Mtukufu:
"Muhamadi ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu" [Surat Al-fath :29]

Jawabu: Neno la Tauhidi ni "Laa ilaaha illa llaahu" Na maana yake: Ni kuwa hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee.
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Basi tambua ya kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu" [Suratu Muhammad: 19]

Jawabu: Mwenyezi Mungu yuko mbinguni juu ya Arshi, yuko juu ya viumbe vyote, Amesema Mtukufu: "Mwingi wa rehema, juu ya 'Arsh Amelingana, yaani Amekuwa juu na Ameangatika, kulingana kunakonasibiana na utukufu Wake na ukubwa Wake." [Suratu Twaha: 5] Na alisema: "Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, Ndiye Mwenye kutenza nguvu, Aliye juu ya waja Wake. Shingo zimemdhalilikia na majabari wamenyongeka Kwake. Yeye Ndiye Mwenye hekima Anayeweka vitu mahali pake kulingana na hekima Yake. Ndiye Mtambuzi Ambaye hakuna kitu chenye kufichikana Kwake". [Suratul An'am: 18].

Jawabu: Maana yake: Ni kuwa Mwenyezi Mungu kamtuma kwa walimwengu wote ili awape habari njema na awaonye.
Na ni wajibu:

1- Kumtii katika yale aliyoyaamrisha.
2- Kumsadikisha katika yale aliyoyaeleza.
3- Kutomuasi.
4- Asiabudiwe Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa yale aliyoyafundisha kama sheria, nako ni kuiga kupitia mafundisho yake (Sunna) na kuacha uzushi.
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Mwenye kumtii Mtume basi hakika atakuwa kamtii Mwenyezi Mungu" [Suratun Nisaa: 80], na akasema Mtukufu "Na hatamki kwa matamanio 3- Bali huo ni ufunuo anafunuliwa" [Surat Najm: 3,4]. Na anasema aliyetakasika na kutukuka: {Hakika nyinyi mna kiigizo chema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anaye mtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja kwa wingi} ((21)), [Suratul Israi: 21].

Jawabu: Alituumba kwa ajili ya kumuabu yeye pekee asiye na mshirika.
Si kwa ajili ya upuuzi wala mchezo.
Amesema Allah Mtukufu:
{Sikuumba majini wala watu ila ni kwa lengo la kuniabudu} (56), [Suratu Dhariyat: 56].

Jawabu: Ni jina linalokusanya yale yote anayoyapenda Mwenyezi Mungu na kuyaridhia katika maneno na matendo ya siri na ya wazi.
Matendo ya wazi:
Mfano kama kumtaja Mwenyezi Mungu kwa ulimi, miongoni mwa tasbihi (kusema Sub-haanallaah) na tahmidi (kusema Alhamdulillaah) na takbiri (kusema Allaahu Akbar) na swala na Hijja.
Matendo ya siri:
Mfano kama kumtegemea Mwenyezi Mungu na kuwa na hofu na matumaini.

Jawabu: Wajibu mkubwa kwetu sisi: Ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Jawabu: 1- Tauhidur rubuubiya (Tauhidi ya ulezi) Nayo ni kuamini kuwa Mwenyezi Mungu ndiye muumbaji, mgawa riziki Mmiliki na mpangiliaji, yeye pekee asiye na mshirika wake.
2- Tauhidul uluuhiyya (Tauhidi ya uungu): Nayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu kwa ibada, asiabudiwe yeyote ila Mwenyezi Mungu Mtukufu.
3- Tauhidul Asmaai wasswifaati (Tauhidi ya majina na sifa): Nayo ni kuyaamini majina na sifa za Mwenyezi Mungu Mtukufu zilizokuja katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na mafundisho ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, bila kupiga mfano wala kushabihisha wala kupotosha.
Na ushahidi wa aina hizi tatu za tauhidi:
Ni kauli yake Mtukufu: «Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake, Ndiye Mmiliki, Muumba na Mwendeshaji wa hivyo vyote, basi muabudu Yeye Peke Yake, ewe Nabii, na uvumilie katika kumtii, wewe na waliokufuata, Hana mfano Wake kitu chochote katika dhati Yake, sifa Zake na vitendo Vyake.» [Suratu Mariam: 65].

Jawabu: Ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na kitu kingine.
Amesema Allah Mtukufu:
"Hakika Mwenyezi Mungu, Hamsamehi aliyemshirikisha Yeye na yeyote miongoni mwa viumbe Wake au akamkufuru kwa aina yoyote ya ukafiri mkubwa. Lakini Anayasamehe na kuyafuta madhambi yaliyo chini ya ushirikina kwa Anayemtaka miongoni mwa waja Wake. Na yeyote anayemshirikisha Mwenyezi Mungu na mwingine, hakika amefanya dhambi kubwa. [Suratun Nisaa: 48]

Jawabu: Ushirikina: Ni kuielekeza aina yoyote miongoni mwa aina za ibada kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Aina zake:

Shirki kubwa; Mfano: Kumuomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, au kumsujudia asiyekuwa yeye Mtakasifu, au kuchinja kwa ajili ya asiyekuwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka.
Shirki ndogo; Mfano:
Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, au mahirizi, nayo ni yale yanayotundikwa kwa ajili ya kuleta manufaa au kuzuia madhara, na shirki ndogo kabisa ni kujionyesha, mfano kama mtu kupendezesha swala yake kwa kuwa anaona kuna watu wanamtazama.

Jawabu: Hakuna ajuaye ghaibu isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee,
Alisema Allah Mtukufu:
"Sema, ewe Mtume, kuwaambia wao, «Hakuna yeyote ajuaye, mbinguni wala ardhini, jambo lolote lililofichikana ambalo Mwenyezi Mungu Amejihusisha Mwenyewe kulijua. Na wao hawajui ni lini watafufuliwa kutoka makaburini mwao wakati wa Kiyama kusimama.» [Suratun Namli: 65]

Jawabu: 1- Kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.
2- Na Malaika wake.
3- Na vitabu vyake.
4- Na Mitume wake.
5- Na siku ya mwisho.
6- Na makadirio kheri yake na shari yake.
Na ushahidi:
Ni hadithi ya Jibrili ambayo ni mashuhuri iko katika sahihi Muslim, alisema Jibrili kumwambia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake. "Basi nieleze kuhusu imani, akasema: Ni kumuamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na vitabu vyake na Mitume wake na siku ya mwisho na kuamini makadirio kheri yake na shari yake."

Jawabu: Kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Ni kumuamini Mwenyezi Mungu kuwa yeye ndiye aliyekuumba na akakuruzuku, na yeye ndiye Mfalme na mpangiliaji peke yake wa viumbe vyote.
Naye ndiye muabudiwa, hakuna muabudiwa kwa haki zaidi yake.
Na kuwa yeye ni Mtukufu Mkuu aliye kamilika Mwenye sifa zote, na ana majina mazuri mno na sifa za hali ya juu, hana mshirika, na hakimfanani chochote Mtukufu.
Kuamini Malaika:

Nao ni viumbe kawaumba Mwenyezi Mungu kwa Nuru, na kwa ajili ya kumuabudu yeye na kwa ajili ya utiifu mkamilifu katika amri zake.
-Miongoni mwao ni Jibrili Amani iwe juu yake anayeteremka na ufunuo (Wahyi) kwa Manabii.
Kuamini vitabu:

Navyo ni vitabu alivyo viteremsha Allah juu Mitume wake.
Kama Qur'ani:
Kwa Muhammad Rehema na Amani ziwe juu yake.
-Injili: kwa Issa- Amani iwe juu yake.
-Taurati: kwa Mussa- Amani iwe juu yake.
-Zaburi: kwa Daudi- Amani iwe juu yake.
-Nyaraka za Ibrahim Amani iwe juu yao: Ibrahim na Mussa.
Kuamini mitume:

Nao ni wale aliowatuma Mwenyezi Mungu kwa waja wake ili wawafundishe, na wawabashirie mazuri na pepo, na wawaonye dhidi ya shari na moto.
-Na wabora wao ni wenye uthubutu, (ulul a'zmi) Nao ni:
Nuhu Amani iwe juu yake.
Ibrahim Amani iwe juu yake.
Mussa Amani iwe juu yake.
Issa Amani iwe juu yake.
Muhammad Rehema na Amani ziwe juu yake.
Kuamini siku ya mwisho:

Nayo ni yale yatakayo kuwa baada ya kifo katika makaburi, na siku ya kiyama, na siku ya kufufuliwa na kuhesabiwa, kiasi ambacho watatulizana watu wa peponi katika makazi yao, na watu motoni katika makazi yao.
Kuamini Makadirio kheri yake na shari yake.
Makadirio:
Ni kuitakidi kuwa Mwenyezi Mungu anajua kila kitu kinachotokea katika ulimwengu, na kuwa yeye alikiandika katika ubao uliohifadhiwa, na akataka kutokea kwake na kukiumba kwake.
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Hakika sisi kila kitu tumekiumba kwa makadirio". [Suratul Qamar: 49].
Nayo yako katika daraja nne:

Daraja ya kwanza: Ni Elimu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na miongoni mwake ni elimu yake iliyokitangulia kila kitu, kabla ya kutokea kwa vitu na baada ya kutokea kwake.
Na ushahidi wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Hakika Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Anajua ni lini Kiyama kitasimama. Na Yeye Ndiye Anayeteremsha mvua kutoka mawinguni, hakuna awezaye hilo yeyote isipokuwa Yeye. Na Anajua vilivyomo ndani ya vizazi vya wanawake. Na Anajua kitakachotendwa na kila mtu wakati ujao. Na hakuna nafsi inayojua itafia wapi. Ni Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Peke Yake Ndiye Anayehusika kwa kujua hayo yote. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi, Ameyazunguka mambo ya nje na ya ndani, hakuna chochote katika hayo kinachofichikana Kwake." [Suratu Luqman: 34].
Daraja ya pili:
Nikuwa Mwenyezi Mungu aliandika hilo katika ubao uliohifadhiwa, kila kitu kilichotokea na kitakachotokea basi kimeandikwa kwake katika kitabu.
Na ushahidi wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
{Na ziko kwake funguo za ghaibu; hakuna azijuaye ila Yeye tu. Na Yeye anajua kilichoko nchi kavu na baharini. Na halidondoki jani ila analijua. Wala punje katika giza la ardhi, wala kinyevu, wala kikavu ila vyote hivyo vimo katika Kitabu kinacho bainisha} (59), [Suratul An'am: 59].
Daraja ya tatu:
Nayo ni kuwa kila kitu kinatokea kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu na wala hakitokei kitu kwake wala kwa viumbe wake isipokuwa ni kwa matakwa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Na ushahidi wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Atakayetaka miongoni mwenu anyooke katika njia. (28) na wala hamuwezi kutaka nyinyi isipokuwa atake Mwenyezi Mungu Mola mlezi wa walimwengu wote (29)" [Suratut takwiri: 28,29]
Daraja ya nne: Ni kuamini kuwa kila kilichopo kimeumbwa, alikiumba Mwenyezi Mungu, na aliumba dhati yake na sifa zake na harakati zake, na kila kitu kinachoambatana nacho.
Na ushahidi wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Na Mwenyezi Mungu amekuumbeni na hayo mnayoyafanya. (96)" [Suratu Swafat: 96].

Jawabu: Ni maneno ya Mwenyezi Mungu mtukufu, hayajaumbwa.
Amesema Allah Mtukufu:
"Na pindi yeyote, miongoni mwa washirikina, akiomba kuingia kwenye himaya yako, ewe Mtume, na akataka amani, basi mkubalie maombi yake ili apate kuyasikia maneno ya Mwenyezi Mungu mtukufu na auone uongofu wake," [Suratu Tauba: 6].

Jawabu: Ni kila kauli au kitendo au kukiri kwake Mtume au sifa ya kimaumbile au kitabia ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.

Jawabu: Ni kila walichokizua watu katika dini, na wala hakikuwepo katika zama za Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake na maswahaba zake.
*Hapana, hatuukubali na tunaukataa.
Kwa kauli yake Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake:
"Kila uzushi ni upotovu" Imepokelewa na Abuu Daud
Na mfano wake: Ni kuongeza katika ibada, kama kuzidisha katika udhu kuosha mara ya nne, na kama kusherehekea kuzaliwa kwa Mtume, haya hayakupokelewa kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake na maswahaba zake.

Jawabu: Kupendana: Ni mapenzi ya waumini na kusaidizana kwao.
Amesema Allah Mtukufu:
{Na Waumini wanaume na Waumini wanawake wao kwa wao ni marafiki}. [Suratu Tauba: 71].
Na kutengana kwa ajili ya Allah:
Ni kuwachukia makafiri na kuwafanyia uadui.
Amesema Allah Mtukufu:
"Hakika imekuwa kwenu nyinyi ni kiigizo chema kwa Ibrahim na wale waliopamoja naye, pale waliposema kuwaambia watu wao; 'Hakika sisi tumejitenga mbali na yale mnayoyaabudu kinyume na Mwenyezi Mungu, tumekupingeni na umedhihiri kati yetu sisi na nyinyi uadui na chuki milele mpaka mumuamini Mwenyezi Mungu peke yake" [Suratul Mumtahina: 4]

Jawabu: Hakubali Mwenyezi Mungu dini isiyokuwa uislamu.
Amesema Allah Mtukufu:
"Na mwenye kuchagua isiyokuwa dini ya kiislamu haitokubaliwa kwake naye Akhera atakuwa ni miongoni mwa waliopata hasara (85)" [Surat Al Imrani: 85]

Jawabu: Mfano wa kauli: Ni kumtukana Mwenyezi Mungu Mtukufu au Mtume wake Rehema na Amani ziwe juu yake.
Mfano wa matendo:
Ni kuudhalilisha msahafu au kumsujudia asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Mfano wa itikadi:
Ni kuitakidi kuwa kuna mwingine anayestahiki kuabudiwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu au kuna muumbaji mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Jawabu:
1- Unafiki mkubwa: Nao ni kuficha ukafiri na kudhihirisha imani.
Na huu unamtoa mtu katika uislamu nao ni katika ukafiri mkubwa.
Amesema Allah Mtukufu:
"Hakika wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa motoni na wala hawatompata yeyote wa kuwanusuru" [Suratun Nisaa: 145]
2- Unafiki mdogo:
Kuongopa na kutotimiza ahadi na kufanya hiyana katika amana.
Na huu haumtoi mtu katika uislamu, nao ni katika madhambi na mfanyaji anajitia katika adhabu.
Amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani ziwe juu yake. "Alama za Mnafiki ni tatu: Anapozungumza husema uongo, na anapoahidi huenda kinyume, na akiaminiwa hufanya hiyana". Ameipokea Bukhari na Muslim.

Jawabu: Ni Muhammad Rehema na Amani ziwe juu yake.
Amesema Allah Mtukufu:
{Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho wa Manabii} [Suratul Ahzaab: 40]. -Na Amesema mjumbe wa Mwenyezi Mungu rehema na Amani ziwe juu yake. "Na mimi ndiye mwisho wa Manabii hakuna Nabii baada yangu" Imepokelewa na Abuu Daud na Tirmidhiy na wengineo.

Jawabu: Muujiza: Ni kila alichokitoa Mwenyezi Mungu kuwapa manabii wake katika mambo ambayo yako nje ya mazoea ya kawaida, ili kuonyesha ukweli wao, mfano:
-Kupasuka mwezi kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.
-N kupasuka kwa Bahari kwa Mussa Amani iwe juu yake, na kuangamizwa Firauni na majeshi yake.

Jawabu: Ni yule aliyekutana na Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake akamuamini na akafa katika uislamu.
-Ndiyo tunawapenda na tunaiga kutoka kwao, nao ni wabora kuliko watu wengine baada ya manabii.
Na wabora wao zaidi ni:
Makhalifa (viongozi) wanne:
Abuu bakari Radhi za Allah ziwe juu yake
Omari -Radhi za Allah ziwe juu yake-
Othman -Radhi za Allah ziwe juu yake-
Ally -Radhi za Allah ziwe juu yake-

Jawabu: Hao ni wake za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-.
Amesema Allah Mtukufu:
"Nabii ni bora zaidi kwa waumini kuliko nafsi zao, na wake zake ni mama zao". [Suratul Ahzab: 6].

Jawabu: Tunawapenda na tunawajali, na tunamchukia mwenye kuwachukia, na wala hatuchupi mipaka kwao, nao ni wake zake na watoto wake na ukoo wa bani Hashim na bani Abdul Muttwalib katika waumini.

Jawabu: Wajibu wetu: Ni kuwaheshimu na kusikiliza na kuwatii katika mambo ambayo si maasi, na kutojitoa katika uongozi wao kwa kuwapinga, na kuwaombea dua na kuwapa nasaha kwa siri.

Jawabu: Ni pepo, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Hakika Mwenyezi Mungu Atawatia, wale ambao waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakajikita katika Imani hiyo na wakafanya mema, kwenye mabustani ya Pepo ambayo inapita mito chini ya majumba yake ya kifahari na miti yake." [Suratu Muhammad: 12]

Jawabu: Ni moto, Amesema Allah Mtukufu: "Basi uogopeni moto ambao kuni zake ni watu na mawe umeandaliwa kwa ajili ya makafiri" [Suratul Baqara: 24].

Jawabu: Hofu: Ni kumuogopa Mwenyezi Mungu na kuogopa adhabu zake.
Kutaraji:
Ni kutaraji thawabu za Mwenyezi Mungu na msamaha wake na rehema zake.
Na ushahidi ni kauli yake Allah Mtukufu:
"Hao washirikina wanawaomba, miongoni mwa Manabii, watu wema na Malaika, wao wenyewe wanashindana kujiweka karibu na Mola wao kwa matendo mema wanayoyaweza, wanatarajia rehema Yake na wanaogopa adhabu Yake. Hakika adhabu ya Mola wako ndiyo ambayo inatakikana kwa waja wawe na tahadhari nayo na waiogope(adhabu ya moto)". [Suratul Israai: 57]. Na amesema Allah Mtukufu: {Wape habari, ewe Mtume, waja wangu kwamba mimi ni mwenye kuwasamehe Waumini wenye kutubia, ni mwenye huruma kwao 49 Na kwamba adhabu yangu ndiyo adhabu iumizayo}. [Suratul Hijri: 49,50].

Jawabu: Allah, Arrabbu (Mola/Mlezi), Assamiiu (Msikivu), Albaswiru (Mwingi wa kuona), Al'aliimu (Mjuzi), Alrazzaq (Mgawa riziki), Al Hayyu (Aliye hai), Al A'adhwiimu (Mtukufu) Na mengineyo katika majina mazuri na sifa za hali ya juu.

Jawabu: Allah: maana yake ni Mola muabudiwa wa kweli, yeye pekee asiye na mshirika wake.
Arrabbu (Bwana): Yaani: Muumba na mmiliki mgawa riziki na mpangiliaji yeye peke yake aliyetukuka.
Assamiiu:
Ambaye usikivu wake umekienea kila kitu, na anazisikia sauti zote pamoja na kutofautiana kwake na kuwa na aina mbali mbali.
Albaswiru:
Anaye kiona kila kitu, na anakiona kila kitu kiwe kidogo au kikubwa.
Al A'liimu:
Naye ni yule ambaye elimu yake imekizunguka kila kitu kilichopita na kilichopo na kijacho.
Alrahman:
Ambaye huruma yake imekienea kila kiumbe na kila kilicho hai, waja wote na viumbe vyote viko chini ya huruma yake.
Arrazzaaq:
Ambaye anajukumu la kugawa riziki kwa viumbe wote kuanzia watu na majini na wanyama wote.
Al hayyu:
Aliye hai ambaye hafi, na viumbe wote wanakufa.
Al A'dhwiim:
Mwenye ukamilifu wote na utukufu wote katika majina yake na sifa zake na vitendo vyake.

Jawabu: Tunatakiwa kuwapenda na kurejea kwao katika maswala mbali mbali na yale yanayotokea katika mambo ya sheria, na hatuwasemi ila kwa mazuri, na mwenye kuwataja kwa mambo tofauti na hayo katika mambo mabaya; basi huyu atakuwa hayuko katika njia sahihi.
Amesema Allah Mtukufu:
"Mwenyezi Mungu Anawapandisha vyeo wale Waumini miongoni mwenu, na Anawapandisha vyeo wale wenye elimu daraja nyingi kwa kuwapatia malipo mema na daraja za kupata radhi. Na Mwenyezi Mungu Anayatambua matendo yenu, hakuna chochote kinachofichikana Kwake katika hayo, na Yeye ni mwenye kuwalipa nyinyi kwayo" {Suratul Mujadila: 11].

Jawabu: Ni waumini wachamungu.
Amesema Allah Mtukufu:
"Tambueni kuwa vipenzi wa Mwenyezi Mungu hawatokuwa na hofu juu yao na wala hawatohuzunika, (62) Wale walioamini na wakawa wachamungu" [Suratu Yunus: 62,63].

Jawabu: Imani ni kauli na matendo na itikadi.

Jawabu: Imani inaongezeka kwa kumtii Mwenyezi Mungu na inapungua kwa kufanya maasi.
Amesema Allah Mtukufu:
"Hakika wenye kumuamini Mwenyezi Mungu ni wale ambao akitajwa Mwenyezi Mungu hulainika nyoyo zao na wasomewapo aya za Mwenyezi Mungu zinawazidishia Imani na kwa Mola wao wanategemea" [surat Anfaal:2]

Jawabu: Ni Kumuabudu Mwenyezi Mungu kana kwamba unamuona na ikiwa humuoni basi Yeye anakuona.

Jawabu: kwa sharti mbili:
1- Yatakapokuwa halisi kwa ajili ya kutaka radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu.
2- Na yatakapokuwa katika mafundisho ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.

Jawabu: Ni kutegemea kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kuleta manufaa na kuondoa madhara, pamoja na kuchukua sababu.
Amesema Mwenyezi mungu Mtukufu:
"Na mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu basi yeye humtosheleza" [Suratu Twalaq: 3.]
Humtosheleza: Yaani: Humtekelezea kila kitu.

Jawabu: Kuamrisha mema: Ni kuamrisha katika kila ambalo ni la kumtii Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, na uovu: Ni kukataza kila maasi ya kumuasi Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka.
Amesema Allah Mtukufu:
"Nyinyi, enyi umma wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni umma bora na ni watu wenye manufaa zaidi kwa watu, mnaamrisha mema, nayo ni yale yanayofahamika uzuri wake kisheria na kiakili, na mnakataza maovu , nayo ni yale yanayoeleweka ubaya wake kisheria na kiakili, na mnamuamini Mwenyezi Mungu kikweli-kweli imani inayotiliwa nguvu na vitendo." [Surat Al Imran: 110]

Jawabu: Ni wale watakaokuwa katika mfano wa yale aliyokuwa nayo Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake na maswahaba zake katika kauli na matendo na itikadi.
Na wameitwa kuwa ni Ahlussunna:
kwa kufuata kwao mafundisho ya Nabii Rehema na Amani ziwe juu yake, na kuacha kuzua.
Na Jama'a:
(Wamoja) Kwa sababu wao walikubaliana katika haki na wala hawakufarakani.