Sehemu ya maamrisho:

Jawabu:
1- Wajibu (Faradhi)
2- Sunna.
3- Haramu.
4- Machukizo (Makruhu).
5- Halali.

Jawabu:
1- Wajibu (Faradhi): Mfano kama swala tano, na kufunga mwezi wa ramadhani, na kuwatendea wema wazazi wawili.
-Jambo la wajibu hulipwa thawabu mfanyaji wake ni huadhibiwa mwenye kuliacha.
2- Sunna: Mfano kama swala za sunna zenye mpangilio (Sunani Rawatibu) Na kisimamo cha usiku, na kulisha chakula, na kutoa salamu, na huitwa sunna au Mandubu.
-Jambo la Sunna hulipwa mfanyaji wake na wala haadhibiwi mwenye kuliacha.
Angalizo muhimu:

Ni lazima kwa kila muislamu anaposikia kuwa jambo hili ni sunna au linapendeza (Mandubu) afanye haraka kulitekeleza, na kumuiga Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.
3- Haramu: Mfano kunywa pombe na kuwaasi wazazi wawili, na kukata udugu.
-Haramu hulipwa mwenye kuiacha na huadhibiwa mwenye kuifanya.
4- Machukizo (Makruhu): Mfano kama kupokea na kutoa au kumpa mtu kwa mkono wa kushoto, na kufunua nguo ndani ya swala.
-Machukizo hupata malipo mwenye kuyaacha na wala haadhibiwi mwenye kuyafanya.
5- Halali: Mfano kama kula tufaa (Apple) na kunywa chai, na huitwa: yanayoruhusiwa au kwa jina jingine halali.
-Mambo ya halali hapati malipo mwenye kuyaacha na wala haadhibiwi mwenye kuyafanya.

Jawabu: Asili katika biashara zote na miamala yote ni halali, isipokuwa baadhi ya aina ambazo kaziharamisha Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Amesema Allah Mtukufu:
"Na amehalalisha Mwenyezi Mungu biashara na akaharamisha riba" [Suratul Baqara: 275].

Jawabu:
1- Ghushi, na miongoni mwake: ni Kuficha aibu za bidhaa.
Na kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake alipita katika gunia la chakula, akaingiza mkono wake ndani yake, vidole vyake vikapata unyevunyevu, akasema: "Ni nini hiki ewe muuza chakula?" Akasema: Kimenyeshewa na mvua ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Akasema: "Kwa nini usikiweke juu ili watu wakione? Yeyote mwenye kudanganya si miongoni mwangu" Imepokelewa na Imamu Muslim
2- Riba: Na miongoni mwake, ni kuchukua deni la elfu moja kwa mtu ili nije kumlipa elfu mbili.
Na ziada ndio riba iliyoharamishwa.
Amesema Allah Mtukufu:
"Na amehalalisha Mwenyezi Mungu biashara na akaharamisha riba" [Suratul Baqara: 275].
3- Udanganyifu na kutoeleweka: Kama kuuza maziwa yakiwa katika chuchu za mnyama, au kuuza samaki wakiwa majini kabla ya kuwavua.
Imekuja katika hadithi:
"Alikataza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake biashara ya udanganyifu" Imepokelewa na Imamu Muslim

Jawabu: 1- Neema ya uislamu, nakuwa wewe si katika watu wapingaji.
2- Neema ya mafundisho ya Mtume (Sunna), nakuwa wewe si miongoni mwa wazushi.
3- Neema ya uzima na afya, kama masikio na macho na kutembea na zinginezo.
4- Neema ya vyakula, vinywaji na mavazi.
Na neema zake Mtukufu juu yetu ni nyingi hazihesabiki wala hazidhibitiki kwa idadi maalumu.
Amesema Allah Mtukufu:
"Na mkijaribu kuzihesabu neema za Mwenyezi Mungu kwenu, ili mjue idadi yake, hamuwezi kuzidhibiti kwa wingi wake na utofauti wake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, ni Mwenye huruma kwenu, kwani Anasamehe kasoro zenu za kutotekeleza ushukuru wa neema, wala Hazikati kwenu, kwa kukiuka kwenu mipaka, wala Hawaharakishii mateso". [Suratun nahli: 18]

Jawabu: La wajibu: Ni kushukuru, na kunakuwa kwa kumsifu Mwenyezi Mungu na kumhimidi kwa ulimi na yakwamba yeye pekee ndiye mwenye fadhila, na kwa kuzitumia neema hizi katika yale yenye kumridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, si kwa kumuasi.

Jawabu: Sikukuu za Fitri na Adh-ha (Iddil Fitri na Iddil Adh-ha)
Kama ilivyokuja katika hadithi ya Anasi, Amesema: Alikuja Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika mji wa Madina akakuta wakiwa na siku mbili ambazo wanazitumia kwa kucheza ndani yake, Akasema: "Ni za nini siku hizi mbili?", Wakasema: Tulikuwa tukicheza ndani yake zama za ujinga, akasema Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake: "Hakika Mwenyezi Mungu amekubadilishieni kwa siku hizo mbili siku bora kuliko hizo: Sikukuu ya Adh-ha, na sikukuu ya Fitri" Kaipokea Abuudaud.
Sikukuu zingine zisizokuwa hizo basi hizo ni katika uzushi.

Jawabu: Mwezi wa ramadhani.

Jawabu: Ni siku ya Ijumaa.

Jawabu: Ni usiku wenye cheo (Lailatul Qadri).

Jawabu: La wajibu ni kuinamisha macho, Amesema Mtukufu: "Sema kuwaambia waumini wa kiume wainamishe macho yao" [Suratun Nuru: 30]

1- Ni nafsi yenye kuamrisha maovu: Nako ni mtu kufuata yale ambayo nafsi yake inamtuma na matamanio yake katika kumuasi Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, Amesema Mtukufu: "Hakika nafsi huamrisha maovu mno, isipokuwa ile ambayo Mola wangu mlezi aliyoirehemu, Hakika Mola wangu Mlezi ni msamehevu na Mwenye kurehemu" [Suratu Yusuf: 53] 2- Shetani: Na huyu ni adui wa mwanadamu, na lengo lake ni kumpoteza na kumtia wasi wasi ili aingie katika shari na amuingize motoni. Amesema Mtukufu: "Na wala msifuate nyayo za shetani, hakika yeye kwenu nyinyi ni adui wa wazi". [Suratul Baqara: 168]. 3- Watu waovu: Wanaohamasisha katika shari, na wanazuia kheri. Amesema Mtukufu: "Marafiki katika kumuasi Mwenyezi Mungu duniani watatengana wao kwa wao Siku ya Kiyama. Lakini wale waliofanya urafiki juu ya uchaji Mwenyezi Mungu, urafiki wao utadumu duniani na Akhera". [Suratuz zukhruf: 67]

Jawabu: Toba: Ni kurudi kutoka katika kumuasi Mwenyezi Mungu Mtukufu kuja katika utiifu. Amesema Mtukufu: "Na mimi ni Mwingi wa kusamehe kwa anayetubia kutokana na dhambi zake na ukanushaji wake, akaniamini mimi na akafanya matendo mema kisha akaongoka kufuata njia ya ukweli na akasimama imara juu yake." [Suratu Twaha: 82]

Jawabu: 1- kujiondoa katika dhambi.
2- Kujuta kwa yaliyopita.
3- Kuazimia kutorudia kosa.
4- Kurudisha haki na mali za dhulma kwa wenye nazo.
Amesema Allah Mtukufu:
"Na wale ambao wakitenda dhambi kubwa au wakizidhulumu nafsi zao kwa kutenda dhambi chini ya hizo, wanaikumbuka ahadi ya Mwenyezi Mungu ya malipo mema kwa wanaomtii na malipo mabaya kwa wanaomuasi na wanaelekea kwa Mola wao hali ya kutubia wakawa wanamuomba Awasamehe madhambi yao na wakawa wana yakini kwamba hapana anayesamehe madhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu. Na wao kwa sababu hiyo hawaendelei kwenye maasi, na wao wanajua kwamba wakitubia Mwenyezi Mungu Atawakubalia toba yao". [Surat Al Imran: 135]

Jawabu: Maana yake Yakwamba wewe unamuomba Mwenyezi Mungu ampe sifa nabii wake Rehema na Amani ziwe juu yake kwa walioko juu.

Jawabu: Ni tasbihi (kumtukuza Mwenyezi Mungu) nako ni kumtakasa yeye aliyetakasika na kutukuka kutokana na kila pungufu na aibu na ovu.

Jawabu: Ni kumsifia Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kumsifu kwa kila sifa ya ukamilifu.

Jawabu: Nikuwa yeye aliyetakasika ni Mkubwa kuliko kila kitu na mtukufu na ni muheshimiwa kuliko kila kitu.

Jawabu: Hakuna ujanja kwa mja wa kutoka hali moja kwenda hali nyingine, na wala hana nguvu juu ya hilo isipokuwa kwa nguvu za Mwenyezi Mungu.

Jawabu: Yaani: Ni mja kuomba kutoka kwa Mola wake ayafute madhambi yake, na azisitiri aibu zake.