Sehemu ya tafsiri:

Jawabu: Suratul Fatiha na tafsiri yake:
Bismillahir Rahmanir Rahiim (1)" kwa jina la mwenyezi mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu "Alhamdulillaahi Rabbil 'aalamiin" Shukurani zote njema anastahiki mola wa viumbe vyote. "Arrahmaanir rahiim" Mwingi wa Rehema na mwenye kurehemu "Maaliki yaumid-diin" mfalme wa siku ya malipo. "Iyyaakana'budu wa iyyaakanastaiin" wewe tu ndiye tunayekuabudu na wewe tu ndiye tunayekuomba msaada . "Ihdinas swiraatwal mustaqiim" Tuongoze njia iliyonyooka. "Swiraatwalladhiina an 'amta a'laihim, ghairil magh dhuubi a'laihim waladh-dhwaalliin" Njia ya wale uliowaneemesha juu yao, na siyo ya wale uliowakasirikia wala ya wale waliopotea. [Suratul- Faatiha 1-7]
Tafsiri:
Imeitwa kuwa ni suratul faatiha (Kifunguzi); kwa sababu ya kukifungua kitabu cha Mwenyezi Mungu kwa sura hiyo.
{Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu} Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Yaani: Naanza kisomo cha Qur'ani, kwa kutaka msaada kwake Mtukufu nikitaka baraka kwa kutaja jina lake.
{Allah}. Yaani: Muabudiwa kwa haki, na haitwi mwingine jina hilo zaidi yake Mtukufu.
{Al- rahmaan}: Yaani: Mwenye huruma ya hali ya juu, na yenye kuwaenea viumbe wake wote.
{Al rahiim} Mwenye kurehemu: Yaani: Mwenye kuwahurumia waumini.
2- {Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu}. Yaani: Aina zote za sifa na ukamilifu ni vya Mwenyezi Mungu peke yake.
3- {Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu} Yaani: Mwenye huruma pana ambazo zimekienea kila kitu, na mwenye huruma endelevu kwa waumini.
4- {Mmiliki wa siku ya malipo} Yaani: Ni siku ya kiyama.
5- {Wewe tu tunakuabudu na wewe tu tunakuomba msaada} Yaani: Tunakuabudu wewe peke yako, na tunakuomba msaada wewe peke yako.
6- {Tuongoze njia iliyonyooka} Nao ni uongofu wa kuongoka katika uislamu na mafundisho ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.
7- {Njia ya wale uliowaneemesha juu yao, sio ya wale waliokasirikiwa wala ya wale waliopotea} Yaani: Njia ya waja wema wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa Manabii na waliowafuata, na si njia ya wakristo wala Mayahudi.
Na ni sunna mtu aseme baada ya kumaliza kuisoma:
(aamin) Yaani: Tukubalie.

Jawabu: Suratuz zalzala na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu." "Na ikatoa vilivyomo ndani yake: kama wafu" "Na akauliza binadamu, kwa babaiko, «leo ardhi ina nini?» "Siku ya Kiyama ardhi itatoa habari ya mambo yaliyofanywa juu yake mazuri na mabaya." "kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ameiamuru itoe habari ya mambo iliyofanyiwa." "Siku hiyo wataondoka kutoka kwenye kisimamo cha Hesabu wakiwa makundi, ili Mwenyezi Mungu Awaonyeshe waliyoyatenda, mazuri na mabaya, na Awalipe kwayo." "Yeyote mwenye kufanya jema uzito wa mdudu chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera." "Na yeyote mwenye kufanya baya uzito wa punje ndogo atayaona malipo yake Akhera." {Suratuz zalzala: 1-8]
Tafsiri:

1- "Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.": Yaani: Itakapotikiswa Ardhi mtikiso mkali utakaotokea siku ya kiyama
2- "Na ikatoa vilivyomo ndani yake: kama wafu" Na Ardhi ikatoa vilivyo ndani ya tumbo lake miongoni mwa wafu na wengineo.
3- "Na akauliza binadamu, kwa babaiko, «Imezukiwa na nini?» Na mwanadamu atasema katika hali ya kubabaika: Ardhi imekuwaje mbona inatikisika na inagonganagongana?!
4- "Siku ya Kiyama ardhi itatoa habari ya mambo iliyofanyiwa ya uzuri na ubaya." Katika siku hiyo kubwa Ardhi itaeleza yale yaliyofanywa juu yake miongoni mwa mazuri na ya shari.
5- "kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ameiamuru itoe habari ya mambo iliyofanyiwa." Kwakuwa Mwenyezi Mungu imefahamisha na akaiamrisha kufanya hivyo.
"Siku hiyo wataondoka kutoka kwenye kisimamo cha Hesabu wakiwa makundi, ili Mwenyezi Mungu Awaonyeshe waliyoyatenda, mazuri na mabaya, na Awalipe kwayo." Katika siku hiyo kubwa ambayo Ardhi itatetemeka ndani yake, watatoka watu kutoka katika kisimamo makundi; Ili wakashuhudie matendo yao waliyoyafanya duniani.
"Yeyote mwenye kufanya jema uzito wa mdudu chungu mdogo atayaona malipo yake Akhera." Atakayefanya kwa uzito wa sisimizi jambo dogo katika matendo ya kheri na wema; ataliona mbele yake.
"Na yeyote mwenye kufanya baya uzito wa punje ndogo atayaona malipo yake Akhera." Na atakayefanya kiasi hicho hicho katika matendo ya shari; basi atakiona mbele yake.

Jawabu: Suratul Aaadiyaati na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda mbio katika njia Yake kumkabili adui, huku wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia." "Wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini." "Wakishambulia wakati wa asubuhi". "Wakirusha vumbi kwa mbio zao." "Wakiwatia kati makundi ya maadui, kwa kuwazunguka kwa vipando vyao, "Hakika binadamu ni mkanushaji sana wa neema za Mola wake." "Na yeye anakubali ukanushaji wake." "Na yeye ana pupa sana ya mali." "Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapo watoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?" "Na (kwani yeye hajui) kuwa yatatolewa yaliyomo ndani ya vifua: mema au maovu?" "Kwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!" [Suratul Aadiyaat: 1-11]
Tafsiri:
"Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda mbio katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia." Ameapa Mwenyezi Mungu kwa Farasi ambao wanakwenda mbio mpaka inasikika sauti ya pumzi zao kwa sababu ya kasi kubwa ya kukimbia.
"Wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini." Na ameapa pia kwa Farasi ambao wanawasha moto kwa kwato zao zinapogusa miamba kwa sababu ya kuikanyaga kwa nguvu.
"Wakishambulia wakati wa asubuhi" Na amewaapia Farasi ambao wanawashambulia maadui wakati wa asubuhi.
"Wakarusha vumbi kwa mbio zao." Yaani: Wakatimua vumbi kwa mbio zao.
"Wakiwatia kati,maadui kuwazunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui" Yaani: Wakalitia kati kwa Farasi zao kundi katika maadui.
"Hakika binadamu ni mkanushaji sana wa neema za Mola wake." Yaani: Hakika mwanadamu ni mchoyo katika mambo mazuri yale anayoyataka kutoka kwake Mola wake.
"Na yeye anakubali ukanushaji wake" Na hakika yeye juu ya kuzuia kwake mambo mazuri ni shahidi, hawezi kulipinga hilo kwa sababu liko wazi.
"Na yeye ana pupa sana ya mali." Yaani: Na hakika yeye ni mkosefu kwa kupenda kwake mali anayoifanyia ubahili.
"Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?" Hivi kwani hajui huyu mwanadamu anayedanganyika na uhai wa Dunia kuwa Mwenyezi Mungu atakapoyafufua makaburi katika wafu na akawatoa kutoka katika Ardhi kwa ajili ya hesabu na malipo kuwa jambo halitokuwa kama anavyodhania?!.
"Na (kwani yeye hajui) kuwa yatatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?" Na yakawekwa wazi na yakabainishwa yaliyoko ndani ya nyoyo miongoni mwa nia na itikadi na mengineyo.
"Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichikana Kwake" Yaani: Hakika Mola wao katika hilo siku hiyo atakuwa na habari, hakuna chochote kitakachofichikana kwake katika matendo ya waja wake, na atawalipa kwayo.

Jawabu: Suratul Qaari'a na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Kiyama chenye kugonga nyoyo za watu" "Ni nini kinachogonga" "Ni kipi kinachokujuza ni kipi kinachogonga?" "Siku hiyo watu watakuwa , kwa wingi wao, kugawanyika kwao na kuzunguka kwao, ni kama panzi walioenea. Nao ni wale wanaojitupa motoni." "Na majabali yatakuwa ni kama pamba yenye rangi tofauti inayochambuliwa kwa mkono ikawa ni mapepe na ikamalizika." "Basi mwenye kuwa mizani ya mema yake ni nzito," "atakuwa kwenye maisha ya kuridhika Peponi." "Ama mwenye kuwa mizani ya mema yake ni nyepesi na mizani ya maovu yake ni nzito" "Basi makazi yake yatakuwa ni moto wa Hawiya" "Ni kipi kinachokujuza ni upi moto wa Hawiya?" "Ni moto mkali" [Suratul Qaria: 1-11]
Tafsiri:
"Kiyama kigongacho" Kiyama kinachogonga nyoyo za watu kwa ukubwa wa vitisho vyake.
"Ni nini kigongacho" Ni muda gani huu ambao utagonga nyoyo za watu kwa ukubwa wa vitisho vyake?!
"Na nini kitakachokujulisha ni kipi kigongacho?" Ni kipi kilichokufahamisha ewe Mtume ni saa gani hii ambayo inagonga nyoyo za watu kwa ukubwa wa vitisho vyake?! Hiyo ni siku ya kiyama.
"Siku hiyo watu watakuwa , kwa wingi wao, kugawanyika kwao na kuzunguka kwao, ni kama panzi walioenea. Nao ni wale wanaojitupa motoni." Siku ambayo itagonga nyoyo za watu watakuwa mfano wa panzi waliotawanyika wanaozagaa huku na kule.
"Na milima itakuwa kama sufi iliyotawanywa" Na itakuwa milima mfano wa sufi iliyochambuliwa kulingana na wepesi wa kupeperuka kwake na kutembea kwake.
"Ama itakayekuwa mizito mizani yake":
Ama ambaye matendo yake mema yatazidi matendo yake mabaya.
"Basi huyo atakuwa katika maisha ya kuridhika":
Yaani atakuwa katika maisha ya kuridhika atakayoyapata peponi.
"Ama itakayekuwa mwepesi mizani yake":
Ama ambaye matendo yake maovu yatazidi matendo yake mema.
"Basi makazi yake ni moto wa Hawiya" Yaani:
Maskani yake na makazi yake siku ya kiyama ni Jahanamu.
"Ni nini kitakachokujulisha ni ipi hiyo Hawiya":
Ni kipi kitakachokufahamisha ewe Mtume ni ipi hiyo?!
"Ni moto mkali": Nao ni moto wenye joto kali.

Jawabu: Suratut Takaathur na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Kumekushughulisheni kutaka wingi" "Kujishughulisha kwenu na hilo kumeendelea mpaka mkawa makaburini na mkazikwa humo." "Siyo namna hii kunatakiwa kuwapumbaze kushindana kwa wingi wa mali. Itawadhihirikia kuwa Nyumba ya Akhera ni bora kwenu." "Kisha tahadharini mtajua mwisho mbaya wa kutojishughulisha na Akhera." "Siyo namna hii inatakiwa iwashughulishe kushindana kwa wingi wa mali. Lau mnajua ukweli, mngalirudi nyuma na mngalishughulika na kuokoa nafsi zenu kutoka kwenye maangamivu." "Hakika bila shaka mtauona moto wa Jahanam" "Kisha mtauona bila shaka!" "Kisha mtaulizwa kuhusu kila aina ya starehe mliyokuwa nayo." [Suratut Takaathur: 1-8]
Tafsiri:
"kumekushughulisheni kutaka wingi": Kumekushughulisheni enyi watu kujifaharisha kwa mali na watoto mkaacha kumtii Mwenyezi Mungu.
"Mkaendelea kujishughulisha kwenu mpaka mkaingia makaburini" Yaani:
Mpaka mkafa mkaingia makaburini mwenu.
"Si hivyo, mtakuja jua" Hamkutakiwa kuwashughulishe huko kujifaharisha kwa hayo mkaacha kumtii Mwenyezi Mungu, mtakuja kujua mwisho wa huko kujishughulisha.
"Kisha, si hivyo, mtakuja jua": Mtakuja jua mwisho wake.
"Si hivyo, lau mngelijua kikweli kweli": Yaani: Kiukweli laiti mngelijua kwa hakika kuwa nyinyi mtafufuliwa mbele ya Mwenyezi Mungu, nakuwa yeye atakulipeni juu ya matendo yenu, kwa kitendo chenu cha kujishughulisha na kujifaharisha kwa mali na watoto.
"Hakika bila shaka mtauona moto wa Jahim" Namuapa Mwenyezi Mungu mtaushuhudia moto siku ya kiyama.
"Kisha hakika mtauona bila shaka" Kisha mtaushuhudia kuushuhudia kwa uhakika kusikokuwa na shaka ndani yake.
"Kisha mtaulizwa kuhusu kila aina ya starehe mliyokuwa nayo." Kisha bila shaka atakuulizeni Mwenyezi Mungu katika siku hiyo juu ya yale aliyokuneemesheni miongoni mwa afya na utajiri na mengineyo.

Jawabu: Suratul Asri na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Na apa kwa wakati wa laasiri" "Hakika wanadamu wako kwenye maangamivu na upungufu". "Isipokuwa wale waliomuamini Mwenyezi Mungu, wakafanya matendo mema, wakausiana wao kwa wao kushikamana na haki, kufanya matendo ya kumtii Mwenyezi Mungu na kusubiri juu yake" [1]. [Suratul Asri: 1-3]
Tafsiri:
"Na apa kwa wakati wa laasiri": Ameapa Mtukufu kwa nyakati.
"kwamba wanadamu wako kwenye maangamivu na upungufu". Yaani: Kila mwanadamu yuko katika mapungufu na maangamivu.
"Isipokuwa wale waliomuamini Mwenyezi Mungu, wakafanya amali njema, wakausiana wao kwa wao kushikamana na haki, kufanya matendo ya kumtii Mwenyezi Mungu na kusubiri juu yake" Isipokuwa yule atakayeamini na akafanya matendo mema, na pamoja na hilo walingania katika haki na wakasubiri juu ya hilo, hawa ndio waliookoka na hasara.

Jawabu: Suratul Humaza na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Shari na maangamivu yatampata kila mwenye kusengenya watu na kuwatukana." "Ambaye hamu yake ni kukusanya mali na kuyahesabu." "Akidhani kuwa mali yake ambayo ameikusanya itampa dhamana ya kuishi milele duniani na kukwepa kuhesabiwa." "Anavyodhania sivyo. Atatiwa ndani ya Moto ambao huvunjavunja kila kinachotiwa." "Ni kipi kinachokujuza ni kipi kinachovunja vunja?" "Huo ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa." "Ambao kwa ukali wake hupenyeza miilini ukafikia kwenye nyoyo." "Moto huo umefungiwa juu yao wakiwa wametiwa minyororo" "Na pingu ndefu ili wasitoke." [Suratul Humaza: 1-9]
Tafsiri:
"Shari na maangamivu yatampata kila mwenye kusengenya watu na kuwatukana." Tatizo kubwa na adhabu kali kwa mtu anayewasengenya watu kwa wingi, na kuwasema vibaya.
"Ambaye hamu yake ni kukusanya mali na kuyahesabu.": Ambaye pupa yake ni kukusanya mali na kuzihesabu, hana malengo mengine zaidi ya hayo.
"Akidhani kuwa mali yake ambayo ameikusanya itampa dhamana ya kuishi milele duniani na kukwepa kuhesabiwa." Anadhani kuwa mali yake aliyoikusanya itamuokoa na mauti, kuwa atabakia milele katika maisha ya dunia.
"Anavyodhania sivyo. Atatiwa ndani ya Moto ambao huvunjavunja kila kinachotiwa." Uhakika si kama anavyofikiria huyu mjinga, Hakika atatupwa katika moto wa Jahanam ambao unagonga na kukivunja kila kinachorushwa ndani yake kwa ukubwa wa ugumu wake.
"Ni kipi kinachokujuza ni kipi kinachovunja vunja?" Na ni kipi kilichokufahamisha ewe Mtume ni upi moto huu ambao unavunjavunja kila kinachotupwa ndani yake?!
"Huo ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa." Huo ni moto wa Mwenyezi Mungu uliochochewa.
"Ambao kwa ukali wake hupenyeza miilini ukafikia kwenye nyoyo." Ambao unapenyeza katika mili ya watu na kufika mpaka katika nyoyo zao.
"Moto huo umefungiwa juu yao wakiwa wametiwa minyororo" Hakika moto huo umefungwa juu ya wale wenye kuadhibiwa ndani yake.
"na pingu ndefu ili wasitoke." Kwa nguzo imara ndefu ili wasiweze kutoka ndani yake.

Jawabu: Suratul Fil na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Je hujui, ewe Mtume, namna Alivyowafanya Mola wako watu wa ndovu: Abraha Mhebeshi na jeshi lake ambalo alikuja nalo ili kuivunja Alkaba tukufu?" "Kwani Hakuijaalia mipango yao mibaya waliyoifanya ni yenye kuvunjika na kupita patupu?" "Na Aliwapelekea makundi yaliyofuatana, ya ndege waliokuwa wakiwatupia wao vijiwe vya udongo mkavu mgumu." Akawapondaponda, wakawa ni kama majani makavu yaliyoliwa na wanyama na halafu kutupwa." [Suratul Fil: 1-5.]
Tafsiri:
"Je hujui, ewe Mtume, namna Alivyowafanya Mola wako watu wa ndovu: Abraha Mhebeshi na jeshi lake ambalo alikuja nalo ili kuivunja Alkaba tukufu?" Hivi hujui ewe Mtume ni jinsi gani alimfanya Mola wako Abraha na watu wa ndovu walipotaka kuibomoa Alkaaba?!
"Kwani Hakuijaalia mipango yao mibaya waliyoifanya ni yenye kuvunjika na kupita patupu?" Aliifanya Mwenyezi Mungu mipango yao mibaya ya kuibomoa kuwa ni hasara, hawakufanikisha walilotamani la kuwaondoa watu katika Alkaaba, na wala hawakufanikisha chochote.
"Na Aliwapelekea makundi yaliyofuatana," Na akawatumia ndege, waliowajia makundi kwa makundi.
ya ndege waliokuwa wakiwatupia wao vijiwe vya udongo mkavu mgumu." Waliwapiga kwa mawe ya udongo mgumu.
Akawapondaponda, wakawa ni kama majani makavu yaliyoliwa na wanyama na halafu kutupwa." Mwenyezi Mungu akawafanya kama majani ya mimea yaliyotafunwa na mnyama na akayakanyaga.

Jawabu: Suratu Quraishi na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
(Kwa ajili ya kuzoea Makuraishi) (1) (Kuzoea kwao misafara ya kusi na kaskazi) (2) "Basi, wamshukuru na kumuabudu Bwana wa Nyumba hii ya Alkaaba, Ambaye kwa ajili Yake wametukuzwa, na wampwekeshe na kumtakasia ibada." "Ambaye Amewapa wao chakula wakati wa njaa kali na akawapa amani na utulivu kutokana na hofu kubwa na mbabaiko." [Suratu Quraishi: 1-4]
Tafsiri:
(Kwa ajili ya kuzoea Makuraishi) (1) Makusudio ya hilo na kile walichokuwa wamekizoea miongoni mwa safari za masika na kiangazi.
(Kuzoea kwao misafara ya kusi na kaskazi) (2) Safari ya masika walikuwa wakienda Yemen, na safari ya kiangazi walikuwa wakienda Sham (Siria, iraq, Jordan, Palestina) wakiwa na amani.
"Basi, wamshukuru na kumuabudu Bwana wa Nyumba hii ya Alkaaba, Ambaye kwa ajili Yake wametukuzwa, na wampwekeshe na kumtakasia ibada." Basi na wamuabudu Mwenyezi Mungu Mola wa nyumba hii peke yake, aliyewafanyia wepesi safari hizi, na wala wasimshirikisha na yeyote.
"Ambaye Amewapa wao chakula wakati wa njaa kali na akawapa amani na utulivu kutokana na hofu kubwa na mbabaiko." Aliyewalisha wakati wa njaa, na akawapa amani na kuwaondolea hofu, kwa kile alicho kiweka katika nyoyo za waarabu kwa sababu ya utukufu wa msikiti mtukufu, basi walikuwa wakiwatukuza wakazi wa maeneo ya msikiti huo mtukufu.

Jawabu: Suratul Maaun na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Je, waiona hali ya yule ambaye akanusha kufufuliwa na kulipwa?" "Huyo ndiye yule anayemkaripia yatima kwa nguvu akimnyima haki yake kwa sababu ya ususuavu wa moyo wake." "Na wala hawahimizi wengine kulisha masikini. Vipi yeye mwenyewe atamlisha?." "Adhabu kali itawathibitikia wenye kusali" (4) "ambao wameghafilika na Swala zao: hawazisimamishi kama ipasavyo wala hawazisali kwa nyakati zake." "Ambao huonyesha watu amali zao za kheri kwa njia ya ria." "Na wanazuia misaada" [Suratul Maauun: 1-7]
Tafsiri:
"Je, waiona hali ya yule ambaye akanusha kufufuliwa na kulipwa?" Je umemfahamu anayekanusha kuwepo malipo na siku ya kiyama?
"Huyo ndiye yule anayemkaripia yatima kwa nguvu akimnyima haki yake kwa sababu ya ususuavu wa moyo wake." Huyo ni yule anayemsukuma yatima kwa ukali anapokuwa na haja.
"Na wala hawahimizi wengine kulisha masikini. Vipi yeye mwenyewe atamlisha?." Na wala haihimizi nafsi yake, wala hamuhimizi mwingine juu ya kulisha masikini.
"Adhabu kali itawathibitikia wenye kusali" (4) Maangamivu na adhabu kwa wenye kuswali.
"ambao wameghafilika na Swala zao:
hawazisimamishi kama ipasavyo wala hawazisali kwa nyakati zake." Ambao huzipuuza swala zao, hawazijali mpaka wakati wake unapomalizika.
"Ambao huonyesha watu amali zao za kheri kwa njia ya ria." Ambao hujionyesha kwa swala zao na matendo yao, hawatakasi matendo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
"Na wanazuia misaada":
Na wanazuia kuwasaidia wengine kwa vitu ambavyo haviwadhuru endapo watawasaidia.

Jawabu: Suratul Kauthar na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Hakika sisi tumekupa, ewe Nabii, kheri nyingi za dunia na Akhera." "Basi, swali na uchinje kwa ajili ya mola wako pekee". "Hakika mwenye kukuchukia wewe na kuyachukia uliyokuja nayo ya uongofu na nuru ndiye aliyekatiwa kila kheri." [Suratul Kauthar: 1-3]
Tafsiri:
"Hakika sisi tumekupa, ewe Nabii, kheri nyingi za dunia na Akhera, miongoni mwazo ni mto wa Kauthar ulioko Peponi ambao pambizo zake ni mahema ya lulu na mchanga wake ni miski." Hakika sisi tumekupa ewe Mtume kheri nyingi, na miongoni mwake ni mto wa kauthar ulioko peponi.
"Basi,swali na uchinje wako kwa ajili ya mola wako
, Peke Yake, pamoja na kutaja jina Lake" Tekeleza shukrani kwa Mwenyezi Mungu kwa neema hii, usali kwa ajili yake peke yeke na uchinje kwa ajili yake, kinyume na vile wanavyofanya washirikina kwa kujikurubisha katika masanamu yao kwa kuyachinjia.
"Hakika mwenye kukuchukia wewe na kuyachukia uliyokuja nayo ya uongofu na nuru ndiye itakayekatika athari yake na yeye mwenyewe kukatiwa kila kheri." Hakika mwenye kukuchukia ndiye aliyekatikiwa na kila kheri, aliyesahaulika ambaye akitajwa anatajwa kwa ubaya.

Jawabu: Suratul Kaafiruun na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Sema, ewe Mtume, kuwaambia waliokufuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake: «Enyi wenye kumkanusha Mwenyezi Mungu!" «Mimi siabudu mnavyoviabudu miongoni mwa masanamu na waungu wa uongo." «Wala nyinyi si wenye kumuabudu ninayemuabudu.» «Wala mimi si mwenye kuabudu mnavyoviabudu miongoni mwa masanamu na waungu wa uongo." «Wala nyinyi si wenye kuabudu mbeleni ninayemuabudu.» «Nyinyi mna dini yenu mnayoiamini na mimi nina Dini yangu ambayo sitaki nyingine.» [Suratul Kaafiruun: 1-6]
Tafsiri:
«Sema, Enyi wenye kumkanusha Mwenyezi Mungu!" Sema, ewe Mtume, kuwaambia waliomkufuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake
«Mimi siabudu mnavyoviabudu miongoni mwa masanamu na waungu wa uongo." Siabudu kwa wakati huu wala wakati ujao mnavyoviabudu miongoni mwa masanamu.
«Wala nyinyi si wenye kumuabudu ninayemuabudu.»
Wala nyinyi hamuabudu ninayemuabudu mimi, naye ni Allah peke yake.
«Wala mimi si mwenye kuabudu mnavyoviabudu miongoni mwa masanamu na waungu wa uongo." Wala mimi siabudu mnavyoviabudu miongoni mwa masanamu.
«Wala nyinyi si wenye kuabudu mbeleni ninayemuabudu.»
Wala nyinyi hamuabudu ninayemuabudu mimi, naye ni Allah peke yake.
«Nyinyi mna dini yenu mnayoiamini na mimi nina Dini yangu ambayo sitaki nyingine.» Nyinyi mna dini yenu mliyoizusha nyinyi wenyewe, na mimi nina dini yangu aliyoiteremsha Mwenyezi Mungu juu yangu.

Jawabu: Suratun Nasri na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Utakapotimia kwako ewe Mtume, ushindi juu ya makafiri wa Kikureshi na ukaufungua mji wa Makkah." "Na ukaona watu wengi wanaingia kwenye Dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi." "Yatakapotokea hayo, jitayarishe kukutana na Mola Wako kwa kumtakasa, kumhimidi na kumuomba msamaha kwa wingi. Kwani Yeye ni Mwingi wa kuwakubalia toba wenye kumsabihi na kumuomba msamaha, kwa kuwasamehe na kuwarehemu." [Suratun Nasri: 1-3]
Tafsiri:
"Utakapotimia kwako ewe Mtume, ushindi juu ya makafiri wa Kikureshi na ukaufungua mji wa Makkah." Utakapokuja msaada wa Mwenyezi Mungu kwa dini yako ewe Mtume- na utukufu wake, na ukatokea ufunguzi wa Mji wa Makka.
"Na ukaona watu wengi wanaingia kwenye Dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi." Na ukawaona watu wakiingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi.
"Yatakapotokea hayo, jitayarishe kukutana na Mola Wako kwa kumtakasa, kumhimidi na kumuomba msamaha kwa wingi. Kwani Yeye ni Mwingi wa kuwakubalia toba wenye kumsabihi na kumuomba msamaha, kwa kuwasamehe na kuwarehemu." Basi tambua kuwa hiyo ni alama ya kukaribia kumalizika kwa muda wa kutumwa kwako, basi mtakase mola wako kwa kumshukuru juu ya neema ya ushindi, na kutake kwake msamaha, hakika yeye ni mwingi wa kukubali toba za waja wake, na kuwasamehe.

Jawabu: Suratul Masad na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Imepata hasara mikono miwili ya Abu Lahab, na yeye mwenyewe ameangamia" "Haikumfaa mali yake wala alichokichuma" "Ataingia kwenye Moto wenye muwako mkali," "Yeye na mke wake ambaye alikuwa akibeba miba na kuiweka kwenye njia anayopita Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ili kumuudhi." "Kwenye shingo yake patakuwa na kamba imara iliyosokotwa; atabebewa nayo kwenye Moto wa Jahanamu, kisha atarushwa nayo mpaka chini." [Suratul Masad: 1-5.]
Tafsiri:
"Imepata hasara mikono miwili ya Abu Lahab, na yeye mwenyewe ameangamia" Imepata asara mikono ya baba yake mdogo na Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, Abuu Lahab bin Abdil Muttwalib kwa hasara aliyoipata ammi yake, kwani alikuwa akimuudhi Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, na zimebatilika juhudi zake.
"Haikumfaa mali yake wala alichokichuma":
Ni kitu gani zimemsaidia mali zake na watoto wake? Hazijamkinga na adhabu, wala hazijamletea rehema.
"Ataingia kwenye Moto wenye muwako mkali," Atauingia siku ya kiyama moto wenye muwako, akichomwa kwa joto lake.
"Yeye na mke wake ambaye alikuwa akibeba miba na kuiweka kwenye njia anayopita Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ili kumuudhi." Na atauingia mkewe mama Jamil aliyekuwa akimuudhi Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, kwa kumtupia miba katika njia yake.
"Kwenye shingo yake patakuwa na kamba imara iliyosokotwa; atabebewa nayo kwenye Moto wa Jahanamu, kisha atarushwa nayo mpaka chini.": Shingoni mwake kuna kamba nzito iliyokazwa atakuwa akikokotwa nayo kwenda motoni.

Jawabu: Suratul Ikhlaswi na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Sema, ewe Mtume, «Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu Aliyepwekeka kwa ustahiki wa kuabudiwa, uumbaji na utakatifu wa Majina na Sifa, Asiye na mshirika katika hayo." "Mwenyezi Mungu ndiye mkusudiwa" (2) «Hakuzaa wala hakuzaliwa" «Wala hakuna yeyote katika viumbe vyake mwenye kufanana wala kushabihiyananaye katika majina yake, sifa zake wala vitendo vyake.» [Suratul Ikhlaswi: 1-4]
Tafsiri:
"Sema, ewe Mtume, «Yeye ndiye Mwenyezi Mungu aliyepwekeka kwa ustahiki wa kuabudiwa, uumbaji na utakatifu wa Majina na Sifa, Asiye na mshirika katika hayo.": Sema ewe Mtume- Yeye ndiye Mwenyezi Mungu hakuna mungu zaidi yake.
"Mwenyezi Mungu tu ndiye mkusudiwa":
Yaani: Hupelekwa kwake shida zote za viumbe.
"Hakuzaa na wala hakuzaliwa":
Hana mtoto Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka na wala hana mzazi.
"Na wala hakuna yeyote anayefanananaye hata mmoja":
Na wala hajawahi kuwa na mfano wake katika viumbe wake.

Jawabu: Suratut Falaq na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
Sema «Najilinda kwa mola wa mapambazuko". «Kutokana na shari la viumbe na udhia wao" «Na shari ya usiku wenye giza jingi uingiapo na ujikitapo na shari na maudhi mbalimbali yaliyomo ndani yake." «Na shari ya wachawi wenye kupuliza kwenye mafundo wanayoyafunga kwa lengo la kuroga." «Na shari ya hasidi mwenye kuchukia watu, anapowahusudu na kuwadhuru, kwa kutaka neema za Mwenyezi Mungu Alizowaneemesha ziwaondokee.» [Suratul Falaq: 1-5].
Tafsiri:

Sema «Najilinda kwa mola wa mapambazuko". Sema ewe Mtume- Najikabidhi kwa Mola muumba wa asubuhi, na ninajiweka karibu kwake.
"Kutokana na shari ya vile alivyoumba":
Kutokana na shari ya vile vyenye kuudhi katika viumbe vyake.
«Na shari ya usiku wenye giza jingi uingiapo na ujikitapo na shari na maudhi mbalimbali yaliyomo ndani yake.": Najikabidhi kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shari ambazo zinajitokeza usiku miongoni mwa wanyama na wezi.
«Na shari ya wachawi wenye kupuliza kwenye mafundo wanayoyafunga kwa lengo la kuroga.": Na ninajikabidhi kwake kutokana na shari za wanga ambao hupuliza katika mafundo wanaporoga.
«Na shari ya hasidi mwenye kuchukia watu, anapowahusudu na kuwadhuru, kwa kutaka neema za Mwenyezi Mungu Alizowaneemesha ziwaondokee.»
Na kutokana na shari za hasidi mwenye kuwachukia watu anapowahusudu juu ya yale aliyowapa Mwenyezi Mungu katika neema, akitaka ziwaondokee, na kuwatia maudhi.

Jawabu: Suratun Nas na tafsiri yake:
Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake.
"Sema, ewe Mtume, «Ninajilinda na kutaka hifadhi kwa Bwana wa watu" "Mfalme wa watu" (2) "Mola wa watu" «Kutokana na udhia wa shetani ambaye hutia watu wasiwasi wanapoghafilika na hujificha atajwapo Mwenyezi Mungu." «Mwenye kupenyeza shari na shaka kwenye vifua vya watu." «Miongoni mwa mashetani wa kijini na kibinadamu.» [Suratun Nas: 1-6]
Tafsiri:
Sema «Najilinda kwa mola wa watu". Sema ewe Mtume- Najikabidhi kwa Mola muumba wa asubuhi, na ninajiweka karibu kwake.
"Mfalme wa watu":
Anafanya maamuzi yoyote kwao kwa ayatakayo, hawana mmiliki mwingine zaidi yake.
"Mola wa watu":
Muabudiwa wao wa haki, hawana muabudiwa wa kweli mwingine zaidi zake.
«Kutokana na udhia wa shetani ambaye hutia watu wasiwasi wanapoghafilika na hujificha atajwapo Mwenyezi Mungu." Kutokana na shari za shetani ambaye anatia wasi wasi wake kwa watu.
«Mwenye kupenyeza shari na shaka kwenye vifua vya watu." Anapenyeza kwa wasi wasi wake katika nyoyo za watu.
«Miongoni mwa mashetani wa kijini na kibinadamu.»
Yaani: Mwenye kutia wasi wasi anakuwa katika binadamu na anakuwa katika majini.