Sehemu ya Adabu za kiislamu:

Jawabu: 1- Kwa kumtukuza yeye aliyetakasika na kutukuka.
2- Kwa kumuabu yeye pekee asiye na mshirika.
3- Kumtii.
4- Kuacha kumuasi.
5- Kumshukuru na kumsifu yeye Mtakasifu juu ya fadhila zake na neema zake ambazo hazihesabiki.
6- Na kusubiri juu ya makadirio yake.

Jawabu: 1- Kwa kumfuata na kuiga kutoka kwake.
2- Kwa kumtii.
3- Kuacha kumuasi.
4- Kumsadikisha katika yale aliyoyaeleza.
5- Kuacha uzushi kwa kuongeza juu ya muongozo wake.
6- Kumpenda zaidi kuliko nafsi na watu wote.
7- Kumuheshimu na kumtetea na kuyatetea mafundisho yake.

Jawabu: 1- Kuwatii wazazi wawili katika yale ambayo si maasi.
2- Kuwahudumia wazazi.
3- Kuwasaidia wazazi.
4- Kukidhi mahitaji ya wazazi.
5- Kuwaombea dua wazazi.
6- Kuwa na adabu wakati wa maongezi; Haitakiwi kusema: "Ahh!", nayo ni kauli ndogo zaidi.
7- Kutabasamu katika uso wa wazazi wawili na wala siyo kukunja sura.
8- Sinyanyui sauti yangu juu ya sauti ya wazazi wawili, na nina wasikiliza, na wala siwakatishi kwa mazungumzo, na wala siwaiti kwa majina yao, bali ninasema: "Baba yangu", "Mama yangu".
9- Ninaomba ruhusa kabla ya kuingia ndani kwa baba yangu na mama yangu wakiwa chumbani.
10- Nabusu kichwa na mkono wa wazazi wawili.

Jawabu: 1- Kwa kuwatembelea ndugu wa karibu kama kaka na dada, na baba mdogo au mkubwa na shangazi, na mjomba, na mama mdogo au mkubwa, na ndugu wengine wa karibu.
2- Kuwafanyia wema kwa kauli na vitendo, na kuwasaidia.
3- Na miongoni mwake ni kuwasiliana nao na kuwauliza hali zao.

Jawabu: 1- Kwa kuwapenda na kuambatana na marafiki wazuri.
2- Ninajiepusha na ninaacha kuambatana na waovu.
3- Ninawasalimia ndugu zangu na ninawapa mikono.
4- Ninawatembelea wanapougua na ninawaombea dua ya shifaa.
5- Na ninamuombea rehema anayepiga chafya.
6- Na ninaitika wito wake anaponiita kwa ajili ya kumtembelea.
7- Ninampa nasaha.
8- Ninamnusuru anapodhulumiwa, na ninamzuia na dhulma.
10- Ninampendelea ndugu yangu muislamu yale ninayoipendelea nafsi yangu.
11- Ninamsaidia anapohitaji msaada wangu.
12- Simfanyii maudhi, kwa kauli na vitendo.
13- Ninahifadhi siri yake.
14- Simtukani, na wala simsengenyi, au kumdharau, au kumuhusudu, na wala simpelelezi, au kumfanyia ghushi.

Jawabu: 1- Ninamfanyia wema jirani kwa kauli na vitendo, na ninamsaidia anapohitaji msaada wangu.
2- Ninampongeza anapokuwa katika furaha ya sikukuu au ndoa na mengineyo.
3- Ninamtembelea anapougua, ninampa pole anapopatwa na msiba.
4- Na ninampelekea kile ninachokipika katika chakula kwa kiasi ninachokiweza.
5- Simpatii maudhi kwa kauli au vitendo.
6- Simsumbui kwa sauti ya juu, au kumpeleleza, na ninamvumilia.

Jawabu: 1- Ninamkubalia anayeniita kwa ajili ya kuwa mgeni kwake.
2- Ninapotaka kumtembelea yeyote ninamtaka idhini na ahadi pia.
3- Ninaomba ruhusa kabla ya kuingia.
4- Sichelewi kumtembelea
5- Na ninainamisha macho kwa watu wa familia yake.
6- Ninamkaribisha mgeni na ninampokea kwa mapokezi mazuri, kwa uso mkunjufu na wenye bashasha, na ninatumia maneno mazuri ya kumkaribisha.
7- Ninamkalisha mgeni mahala pazuri.
8- Ninamkirimu kwa ugeni wake, katika chakula na vinywaji.

Jawabu: 1- Ninapohisi maumivu; ninaweka mkono wangu wa kulia sehemu inayouma, na ninasema: "Bismillaah" Mara tatu, na ninasema: "Audhu bi izzatillaahi waquduratihi min sharri maa ajidu wa uhaadhir" Mara saba, yaani: Ninajilinda kwa utukufu wa Mwenyezi Mungu na uwezo wake kutokana na shari za yale ninayoyapata na ninachukua hadhari.
2- Ninaridhika na yale aliyoyakadiria na Mwenyezi Mungu na ninasubiri.
3- Ninafanya haraka kumtembelea ndugu yangu akiwa mgonjwa, na ninamuombea dua, na wala sikai kwake muda mrefu.
4- Ninamfanyia kisomo bila ya yeye kuniomba.
5- Ninamuhusia kuvumilia, kuomba dua, kuswali, na kuwa twahara kwa kadiri awezavyo.
6- Dua ya mgonjwa: "As alullaahal Adhwiim Rabbal Arshil Adhwiim an yash-fiyaka" Mara saba, Yaani: Namuomba Allah Mtukufu, Mola wa Arshi Tukufu akuponye.

Jawabu: 1- Kutakasa nia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka.
2- Naifanyia kazi elimu niliyojifunza.
3- Namuheshimu mwalimu na ninampa daraja yake anapokuwepo na anapokuwa hayupo.
4- Nakaa mbele yake kwa adabu.
5- Nanyamaza na kumsikiliza vizuri, na wala simkatishi katika somo lake.
6- Ninakuwa na adabu ninapouliza swali.
7- Simuiti kwa jina lake.

Jawabu: 1- Nawasalimia walioko katika kikao.
2- Na ninakaa pale kinapoishia kikao, simnyanyui yeyote mahali alipokaa wala sikai kati ya watu wawili isipokuwa kwa idhini yao.
3- Ninaacha nafasi katika kikao ili akae mtu mwingine.
4- Sikatishi mazungumzo ya kikao.
5- Ninaomba idhini na ninatoa salamu kabla ya kuondoka katika kikao.
6- Kinapomalizika kikao ninaomba dua ya kafara ya kikao. Sub-haanakallaahumma, wabihamdika, Ash-hadu an laa ilaaha illaa anta, Astaghfiruka wa atuubu ilaika, maana yake " Umetakasika ewe Mwezi mungu, na sifa njema ni zako, nashuhudia kuwa hakuna mola anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa ni wewe, ninakuomba msamaha na ninatubia kwako).

Jawabu: 1- Nalala mapema.
2- Nalala na twahara.
3- Silalii tumbo.
4- Ninalalia ubavu wangu wa kulia, na ninaweka mkono wangu wa kulia chini ya shavu langu la kulia.
5- Ninakung'unta na kutandika kitanda changu.
6- Ninasoma nyiradi za kulala, kuanzia ayatul kursiy, suratul ikhlaswi, na sura za kinga mbili (Suratul falaq na suratun nas) mara tatu tatu, na ninasema: "Bismikallaahumma amuutu wa ahya" Yaani: Kwa jina lako Mola wangu ninakufa, na ninakuwa hai.
7- Naamka kwa ajili ya swala ya alfajiri.
8- Na ninasema baada ya kuamka kutoka usingizini: "Alhamdulillaahi lladhi ah-yaanaa baada maa amaatanaa wailaihin nushuur" Yaani: Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyetuhuisha baada ya kutufisha na kwake tutafufuliwa.

Jawabu:
1- Ninanuia kwa kula kwangu na kunywa kwangu nipate nguvu ya kumtii Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka.
2- Kuosha mikono miwili kabla ya kula.
3- Ninasema: "Bismillah", Na ninakula kwa mkono wangu wa kulia na kwa chakula kilicho mbele yangu, na wala sili katikati ya sahani, au mbele ya mwenzangu.
4- Nikisahau bismillah ninasema: "Bismillahi awwaluhu wa aakhiruhu", kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzo wake na mwisho wake.
5- Ninaridhika na chakula kinachopatikana, na wala sikitoi dosari chakula, kinaponifurahisha nakula, na kisiponifurahisha nakiacha.
6- Ninakula matonge kadhaa tu, na wala sili sana.
7- Na wala sipulizi chakula au kinywaji, na ninakiacha mpaka kipoe.
8- Ninakaa pamoja na watu wengine kwenye chakula, pamoja na familia au mgeni.
9- Sianzi kula chakula kabla ya wenzangu ambao ni wakubwa kuliko mimi.
10- Ninamtaja Mwenyezi Mungu wakati ninapokunywa, na ninakunywa nikiwa nimekaa kwa mafundo matatu.
11- Ninamshukuru Mwenyezi Mungu wakati ninapomaliza kula.

Jawabu: 1- Ninaanza kuvaa nguo yangu kuanzia kulia, na ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hilo.
2- Sirefushi nguo yangu mpaka chini ya kongo mbili za miguu.
3- Hawavai watoto wa kiume nguo za watoto wa kike, wala wa kike nguo za kiume.
4- Kutokujifananisha na mavazi ya makafiri au watu waovu kama wasanii.
5- Kusema bismillah wakati wa kuvua nguo.
6- Kuvaa kiatu cha kulia kwanza, na kuvua kuanzia kushoto.

Jawabu: 1- Ninasema: "Bismillah, Ahamdulillaah", «Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Aliyetudhalilishia (kipando) hiki, na hatukuwa ni wenye uwezo juu yake.» «Na sisi baada ya kufa kwetu ni wenye kuelekea Kwake na kurejea." [Suratuz zukhruf: 13,14].
2- Ninapopita kwa muislamu; ninamtolea salamu.

Jawabu: 1- Ninatembea sawa na ninakuwa mnyenyekevu wakati wa kutembea, na ninatembelea upande wa kulia wa njia.
2- Ninamtolea salamu ninayekutananaye.
3- Ninainamisha macho yangu na wala simuudhi yeyote.
4- Ninaamrisha Mema Na Kukataza Mabaya:
5- Ninaondoa udhia njiani.

Jawabu: 1- Ninatoka kwa mguu wangu wa kushoto na ninasema: (Kwa jina la Mwenyezi Mungu,nimemtegemea kwa Mwenyezi Mungu na hakuna hila (namna) wala nguvu isipokuwa kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, Ewe Mola wangu wa haki hakika mimi najikinga kwako ili nisipotee au kupotezwa au kuteleza na kufanyakosa au kutelezeshwa na kufanya makosa au kudhulumu au kudhulumiwa au kudanganya au kudanganywa mimi) 2- Ninaingia ndani kwa mguu wangu wa kulia, na ninasema: "Bismillah walajinaa, wabismillahi kharajinaa, wa a'laa Rabbinaa tawakkalna" Kwa jina la Mwenyezi Mungu tumerejea, na kwa jina la Mwenyezi Mungu tulitoka, na kwa Mola wetu ndiko tunako tegemea.
3- Naaanza kuswaki kisha ninawasalimia walioko nyumbani.

Jawabu: 1- Ninaingia kwa mguu wangu wa kushoto.
2- Na ninasema kabla ya kuingia: Allaahumma inni audhubika minal khubuthi wal khabaa ithi": "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwako kutokana na mashetani wa kiume na mashetani wa kike."
3- Singii kitu chochote ambacho ndani yake ametajwa Mwenyezi Mungu.
4- Ninajisitiri wakati wa kukidhi haja.
5- Sizungumzi sehemu ya kukidhi haja.
6- Sielekei kibla, na wala sikipi mgongo wakati wa kukidhi haja ndogo au kubwa.
7- Ninatumia mkono wangu wa kushoto katika kuondoa najisi, na wala situmii mkono wa kulia.
8- Sikidhi haja yangu katika njia ya watu au kivuli chao.
9- Ninaosha mkono wangu baada ya kukidhi haja.
10- Ninatoka kwa mguu wangu wa kushoto na ninasema: "Ghufraanaka" Msamaha unatoka kwako.

Jawabu: 1- Ninaingia msikitini kwa mguu wangu wa kulia, na ninasema: "Bismillaah, Allahummaftah li Abwaba rahmatika" Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Ewe Mola nifungulie milango ya rehema zako.
2- Sikai mpaka niswali rakaa mbili.
3- Sipiti mbele ya mwenye kuswali, au kutangaza kilichopotea msikitini, au kuuza au kununua msikitini.
4- Ninatoka msikitini kwa mguu wangu wa kushoto, na ninasema: "Allahumma inni as aluka minfadhlika". Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba unipe katika fadhila zako.

Jawabu: 1- Ninapokutana na muislamu naanza kumsalimia, kwa kauli: "Assalaamu alaikum warahmatullaahi wabarakaatuh" wala siachi kutoa salamu, na wala simuashirii kwa mkono pekee.
2- Ninatabasamu katika uso wa ninayemsalimia.
3- Ninampa mkono wangu wa kulia.
4- Anaponisalimia yeyote kwa salamu ninamjibu kwa uzuri zaidi kuliko alivyonisalimia, au ninamjibu kwa mfano wa alivyosalimia.
5- Simuanzi kafiri kwa salamu, na akinisalimia ninamjibu kama alivyonisalimia.
6- Na mdogo anamsalimia mkubwa, na aliyepanda anamsalimia mtembea kwa miguu, na mtembea kwa miguu anamsalimia aliyekaa, na wachache wanawasalimia wengi.

Jawabu: 1- Ninaomba idhini kabla ya kuingia mahali.
2- Ninaomba idhini mara tatu na wala sizidishi, na baada ya hapo ninaondoka.
3- Ninagonga mlango taratibu, na wala sisimami mbele ya mlango, bali nasimama kuliani kwake au kushotoni kwake.
4- Singii kwa baba yangu na mama yangu au chumba chochote kabla ya kuomba idhini, na hasa hasa kabla ya alfajiri na wakati wa kupumzika mchana (Qailula), na baada ya swala ya ishaa.
5- Ninaweza kuingia sehemu zisizoishi watu, mfano kama Hospitali au majumba ya biashara bila kuomba idhini.

Jawabu: 1- Ninawalisha wanyama na ninawanywesha.
2- Kuwahurumia, kuwafanyia upole wanyama, na kutokuwabebesha mizigo wasiyoiweza.
3- Siwaadhibu wanyama kwa aina yoyote ya adhabu na maudhi.

Jawabu: 1- Ninanuia kwa michezo hii kupata nguvu kwa ajili ya kumtii Mwenyezi Mungu na kumridhisha.
2- Hatuchezi wakati wa swala.
3- Watoto wa kiume hawachezi na watoto wa kike.
4- Ninavaa mavazi ya michezo yenye kusitiri uchi.
5- Ninajiepusha na michezo iliyoharamishwa, kama ambayo ndani yake kuna kupiga uso na kufunua uchi.

Jawabu: 1- Ukweli katika mizaha na kutokuwa muongo.
2- Mizaha iliyoepukana na kejeli, kudhihaki, kumuudhi mtu na kumtisha.
3- Kutokuzidisha mizaha.

Jawabu: 1- Kuweka mkono au nguo au kitambaa wakati wa kupiga chafya.
2- Kumshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kupiga chafya kwa kusema: "Alhamdulilllah"
3- Na aliyemsikia aseme kumwambia ndugu yake: "Yar-hamukallaah" Mwenyezi Mungu akuhurumie.
Akisema kumwambia hivyo:
Basi naye aseme: "Yah-diikumullaahu wayuslih baalakum" Akuongozeni Mwenyezi Mungu na akutengenezeeni mambo yenu".

Jawabu: 1- Kujitahidi kuzuia mwayo.
2- Kutonyanyua sauti kwa kusema: "Aaah" Aaah".
3- Kuweka mkono juu ya mdomo.

Jawabu: 1- Kusoma nikiwa na twahara baada ya kutia udhu.
2- Kukaa kwa adabu na heshima.
3- Ninaomba kinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani mwanzo wa kusoma.
4- Ninazingatia kisomo.