Sehemu ya Historia ya Bwana Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake:

Jawabu: Naye ni Muhammadi bin Abdillah bin Abil Muttwalib bin Hashim, Na Hashim ni katika makuraishi, na makuraishi ni katika waarabu, na waarabu wanatokana na kizazi cha Ismaili bin Ibrahim kipenzi wa Mwenyezi Mungu kwake na kwa Nabii wetu Amani iwe juu yao.

Jawabu: Alifarikia baba yake katika mji wa Madina naye (Mtume) akiwa bado ni ujauzito, hajazaliwa Rehema na Amani ziwe juu yake.

Jawabu: Katika mwaka wa tembo, siku ya juma tatu mwezi wa Rabi'il Awwal (Mwezi wa tatu katika kalenda ya kiislamu)

Jawabu: katika mji wa Makka.

Jawabu: Aliyeachwa huru na baba yake Mama Ayman.
-Aliyeachwa huru na baba yake mdogo Abuu Lahab, Thuwaiba.
-Halimat Sa'diyya.

Jawabu: Alifariki mama yake naye akiwa na umri wa miaka sita, na akamlea babu yake Abdul Muttwalib.

Jawabu: Alifariki babu yake Abdul Muttwalib naye akiwa ni kijana wa umri wa miaka minane, na akalelewa na baba yake mdogo Abuu Twalib.

Jawabu: Alisafiri pamoja na baba yake mdogo kwenda Sham na umri wake ukiwa ni miaka kumi na mbili.

Jawabu: Ilikuwa safari yake ya pili ni katika biashara kupitia mali ya bi Khadija Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, na aliporudi kutoka safari alimuoa bi khadija, naye akiwa na umri wa miaka ishirini na tano.

Jawabu: Walirudishia Makuraishi ujenzi wa Alka'aba, naye akiwa na umri wa miaka thelathini na tano.
Na wakamfanya kuwa hakimu walipotofautiana katika kuliweka jiwe jeusi, akaliweka katika nguo yake, na akaliamrisha kila kabila lishike ncha ya nguo, na yalikuwa makabila manne, walipolinyanyua mpaka mahala pake, akaliweka mwenyewe kwa mkono wake -Rehema na Amani ziwe juu yake.

Jawabu: Umri wake ulikuwa ni miaka arobaini, na alitumwa kwa watu wote, akiwa mtoa habari njema na muonyaji.

Jawabu: Ulianza kwa ndoto za kweli, akawa haoni ndoto isipokuwa ilikuwa ikija mfano wa wingu la asubuhi (ikitokea wazi)

Jawabu: Alikuwa akifanya ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu katika pango la mlima Hiraa, na alikuwa akichukua chakula cha kumtosha kwa ajili ya hilo.
Na ulimteremkia wahyi, naye akiwa katika pango akifanya ibada.

Jawabu: Ni kauli yake Mtukufu: "Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba." "Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu." "Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu." "Aliyewafundisha viumbe wake kuandika kwa kalamu." "Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu." [Suratul A'laq: 1-5].

Jawabu: katika wanaume: Ni Abuubakari swiddiq, na katika wanawake: Ni Khadija binti Khuwailidi, na katika watoto: ni Ally bin Abii Twalib, na katika waachwa huru: Ni Zaidi bin Haritha, na katika watumwa: Ni Bilali Muhabeshi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, na wengineo.

Jawabu: Ujumbe wa uislamu ulikuwa kwa siri kwa takribani miaka mitatu, kisha akaamrishwa Rehema na amani ziwe juu yake kutangaza ujumbe wazi.

Jawabu: Washirikina walipita kiasi katika kumuudhi na kuwaudhi waislamu, mpaka akawaruhusu waumini kuhama kwenda kwa Mfalme Najashi huko Habasha (Ethiopia).
Na wakakubaliana washirikina wote juu ya kumuudhi na kumuua Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, Mwenyezi Mungu akamuhami na akampa ulinzi kupitia baba yake mdogo Abuu Twalib ili amlinde kutokana nao.

Jawabu: Alifariki baba yake mdogo Abuu twalib, na mke wake bi Khadija Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Jawabu: Alikuwa katika umri wa miaka hamsini, na akafaradhishiwa juu yake swala tano.
Israa (Safari ya usiku): Ilikuwa ni kutoka Msikiti mtukufu wa Makka kwenda Msikiti wa Aqswa (palestina)
(Miiraji) Na kupandishwa: kulikuwa ni kuanzia Msikiti wa Aqswa (Palestina) mpaka katika mbingu ya saba mpaka katika mti wa mkunazi wa mafikio ya mwisho (Sidiratul Muntaha).

Jawabu: Alikuwa akiwalingania watu wa Twaifu, na akijitokeza kwao katika misimu mbali mbali na sehemu za mikusanyiko ya watu, mpaka akawaendea watu wa Madina miongoni mwa wale waliomtetea (Maanswari), wakamuamini Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, na wakampa ahadi ya kumnusuru.

Jawabu: Alifaradhishiwa juu yake zaka, na swaumu,na Hijja, na Jihadi, na Adhana, na mengineyo miongoni mwa sheria za uislamu.

Jawabu: Ni vita vikuu vya Badri.
Vita vya Uhudi.
Vita vya makundi (Ahzab)
Vita vya ufunguzi wa Makka (Fat-hu Makka)

Jawabu: Ni kauli yake Mtukufu: "Na itahadharini, enyi watu, Siku mtakaporejeshwa kwa Mwenyezi Mungu, nayo ni Siku ya Kiyama, mtakapo orodheshwa kwa Mwenyezi Mungu ili Awahesabu na Amlipe kila mmoja miongoni mwenu kwa alilolitenda la kheri au la shari bila ya kufikiwa na maonevu" [Suratul Baqara: 281].

Jawabu: Alifariki katika mwezi wa rabiil Awwal, katika mwaka wa kumi na moja tangu kuhamia Madina, akiwa na umri wa miaka sitini na tatu.

Jawabu: 1- Khadija binti Khuwailid Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.
2- Sauda binti Zam'a Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.
3- Aisha binti Abuu Bakari Asswidiiq -Radhi za Allah ziwe juu yake-
4- Hafswa binti Omari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.
5- Zainab bint Khuzaima -Radhi za Allah ziwe juu yake.
6- Ummu Salama, Hindu binti Abii Umaiyya Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.
7- Ummu Habiba Ramla bint Abii Sufiyaan -Radhi za Allah ziwe juu yake-
8- Juweyriyah bint Al Haarithi - Radhi za Allah ziwe juu yake.
9- Maymuunah bint Al Haarithi - Radhi za Allah ziwe juu yake.
10- Swafiyyah bint Huyeyyi - Radhi za Allah ziwe juu yake.
11- Zainab binti Jahshi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.

Jawabu: Katika watoto wa kiume ni watatu:
Qassim, na kwa mtoto huyu alikuwa akiitwa.
Na Abdallah.
Na Ibrahim.
Na katika watoto wa kike:

Fatma.
Rukaiyya.
Ummu Kulthum.
Zainab.
Na watoto wake wote hao walizaliwa na Khadija Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, isipokuwa Ibrahim, na wote walifariki kabla yake isipokuwa Fatma alifariki baada yake kwa miezi sita.

Jawabu: Alikuwa Rehema na Amani ziwe juu yake ni wa kati na kati baina ya wanaume, si mfupi wala si mrefu bali alikuwa kati na kati, na alikuwa mweupe aliyechanganyikana na wekundu Rehema na Amani ziwe juu yake, na alikuwa na ndevu nyingi, mwenye macho mapana, mwenye mdomo mzito, na nywele zake zilikuwa nyeusi sana, mwenye mabega mazito, mwenye harufu nzuri, na zinginezo miongoni mwa sifa zake nzuri Rehema na Amani ziwe juu yake.

Jawabu: Kauacha umma wake Rehema na Amani ziwe juu yake katika njia nyeupe iliyonyooka, usiku wake ni kama mchana wake, hakuna atakayepotoka katika njia hiyo isipokuwa ataangamia, hakuacha kheri yoyote isipokuwa aliujulisha umma wake katika kheri hiyo, wala shari yoyote isipokuwa aliutahadharisha umma na shari hiyo.